Simba yawasili Lubumbashi

Msafara wa kikosi cha Simba uliondoka mapema leo jijini Dar es salaam kuelekea DR Congo, umewasili salama katika mji wa Lubumbashi yalipo makazi ya klabu ya TP Mazembe

Kesho Jumamosi Simba itashuka dimba la Mazembe kuwakabili wenyeji wao katika mchezo wa pili wa robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Simba imetumia usafiri wa Ndege Maalum ya kukodi na wataitumia Ndege hiyo kurejea nchini kesho baada ya mchezo

Mabingwa hao wa Tanzania leo jioni wanatarajia kujifua katika uwanja wa Mazembe ambao utatumika kwenye mchezo wa kesho