
Katika kipindi cha wiki mbili hivi Kagere huenda akajiimarisha kileleni katika mbio hizo kwani Simba itacheza michezo saba ya viporo
Leo Kagere ameiongoza Simba kuondoka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union na kuiweka Simba katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa hasa baada ya Yanga kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mtibwa Sugar
Simba inaelekea mkoani Kagera tayari kwa mchezo mwingine wa kiporo dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa Jumamosi, April 20 2019 katika dimba la Kaitaba