Kagere amfikia Aiyee, afikisha mabao 16 ligi kuu

Mabao mawili aliyofunga Meddie Kagere leo, yamemuwezesha kufikisha mabao 16 na kumfikia Salim Aiyee ambaye amekuwa akiongoza kwa muda mrefu mbio za kuwania kiatu cha dhahabu

Katika kipindi cha wiki mbili hivi Kagere huenda akajiimarisha kileleni katika mbio hizo kwani Simba itacheza michezo saba ya viporo

Leo Kagere ameiongoza Simba kuondoka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union na kuiweka Simba katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa hasa baada ya Yanga kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mtibwa Sugar

Simba inaelekea mkoani Kagera tayari kwa mchezo mwingine wa kiporo dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa Jumamosi, April 20 2019 katika dimba la Kaitaba