Baada ya ushindi Tanga, Simba kurejea Dar

Baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union leo, kikosi cha Simba kinarejea jijini Dar es salaam tayari kuifuata Kagera Sugar

Simba itacheza na Kagera Sugar Jumamosi April 20 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Kaitaba

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema licha ya kukabiliwa na ratiba isiyo rafiki watapambana kuhakikisha wanapata matokeo

Akizungumzia matokeo ya mchezo wa leo, Aussems amewapongeza wachezaji kwa kupata ushindi licha ya mazingira yasiyo rafiki ya uwanja wa Mkwakwani

“Haikuwa rahisi sababu uwanja haukuwa mzuri lakini tulifanikiwa kumiliki mchezo na baadae tulifanya mabadiliko ambayo yametuletea magoli. Kubwa zaidi nawapongeza wachezaji kwa kuibuka na ushindi”