
Simba itacheza na Kagera Sugar Jumamosi April 20 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Kaitaba
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema licha ya kukabiliwa na ratiba isiyo rafiki watapambana kuhakikisha wanapata matokeo
Akizungumzia matokeo ya mchezo wa leo, Aussems amewapongeza wachezaji kwa kupata ushindi licha ya mazingira yasiyo rafiki ya uwanja wa Mkwakwani
“Haikuwa rahisi sababu uwanja haukuwa mzuri lakini tulifanikiwa kumiliki mchezo na baadae tulifanya mabadiliko ambayo yametuletea magoli. Kubwa zaidi nawapongeza wachezaji kwa kuibuka na ushindi”