
Kabwili aliyejiunga na Yanga mwaka juzi baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya AFCON U17 iliyofanyika Gabon, mkataba wake na Yanga uko ukingoni na atakuwa huru ifikapo mwezi Juni
Kabwili amepata nafasi ya kucheza zaidi msimu huu baada ya aliyekuwa mlinda lango namba moja Beno Kakolanya kuingia kwenye mgogoro na kocha Mwinyi Zahera
Kwa sasa hapati nafasi mara kwa mara baada ya mlinda lango aliyeimarisha kiwango chake Klaus Kindoki kumpiku
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amepania kukijenga upya kikosi cha Yanga kwa ajili ya msimu ujao na inaelezwa amewaruhusu wachezaji wote wanaotaka kuondoka, waondoke
Yanga huenda ikamsajili mlinda lango wa Bandari Fc, Farouk Shikalo ambaye usajili wake ulipaswa kukamilishwa mwezi Disemba wakati wa dirisha dogo la usajili kabla ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Yanga Hussein Nyika kushindwa kwenye dakika za majeruhi
Shikalo ni miongoni mwa wachezaji wanne ambao Zahera alisikitika kuwakosa katika usajili huo