
Yanga imesalia na michezo sita kumaliza msimu huku imchezo mmoja dhidi ya Biashara United ukitarajiwa kupigwa nje ya Dar
Yanga itarejea jijini Dar es salaam kutumia uwanja wa Taifa baada ya kumalizika fainali za AFCON U17 April 28 2019
Zahera amesema watahakikisha wanashinda michezo yote iliyobaki pamoja na kuweka msisitizo zaidi kwenye michuano ya kombe la FA (ASFC) wakitarajia kucheza na Lipuli Fc mwanzoni mwa mwezi wa tano katika mchezo wa nusu fainali
“Unajua mimi nimezunguka nchi nyingi sana Afrika lakini sijawahi kuona maamuzi ya hovyo kama ya waamuzi wa Ligi ya Tanzania, Hakuna haki na kungekuwa na haki nina uhakika sasaivi tungekuwa tushajihakikishia ubingwa”
“Kwa sasa tumesahau yote, tunajipanga kuelekea michezo inayofuata ukiwemo wa Azam Fc ili kuhakikisha tunashinda mechi zote zilizosalia huku tukihakikisha tunatwaa ubingwa wa Kombe la ASFC ili kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani”