Simba yarejea Dar usiku kwa usiku, tayari kwa safari ya Kanda ya Ziwa

Kikosi cha Simba kimerejea jijini Dar es salaam usiku kikitokea Tanga ambapo jana kilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union

Kutokana na ukaribu wa michezo yake Simba imelazimika kusafiri usiku na mchana ili kwendana na ratiba ya viporo iliyopangwa na Bodi ya Ligi

Simba inaelekea Kanda ya Ziwa ambapo keshokutwa Jumamosi, April 20 2019 itakuwa dimba la Kaitaba kuikabili Kagera Sugar