Simba kurudi ‘machinjioni’ baada ya AFCON U17 kumalizika

Michuano ya vijana ya AFCON U17 inayoendelea jijini Dar es salaam, inatarajiwa kumalizika April 28 2019 kwa mchezo wa fainali kupigwa ambapo baada ya mchezo huo, uwanja wa Taifa utaruhusiwa kwa matumizi ya michezo ya ligi

Hii ni taarifa njema sana kwa Simba ambayo katika kipindi cha wiki mbili zijazo inakabiliwa na michezo mingi ya viporo inayopigwa ugenini

Mwanzoni mwa mwezi wa tano Simba itarejea kumalizia michezo iliyobaki katika uwanja wa Taifa ambao umepachikwa jina la ‘machinjioni’

Msimu huu Simba imeweka rekodi ya kipekee uwanja wa Taifa kwa kushinda michezo yote iliyocheza kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kulazimishwa sare michezo miwili tu kwenye ligi