
Hii ni taarifa njema sana kwa Simba ambayo katika kipindi cha wiki mbili zijazo inakabiliwa na michezo mingi ya viporo inayopigwa ugenini
Mwanzoni mwa mwezi wa tano Simba itarejea kumalizia michezo iliyobaki katika uwanja wa Taifa ambao umepachikwa jina la ‘machinjioni’
Msimu huu Simba imeweka rekodi ya kipekee uwanja wa Taifa kwa kushinda michezo yote iliyocheza kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kulazimishwa sare michezo miwili tu kwenye ligi