Yanga, Azam Fc zairahisishia Simba mbio za ubingwa

Azam Fc imeangukia pua mkoani Mtwara baada ya kuchapwa bao 1-0 na Ndanda Fc katika mchezo uliopigwa uwanja wa Nangwanda Sijaona

Ndanda Fc pia ilipata alama moja moja kwenye michezo dhidi ya Yanga na Simba iliyopigwa katika uwanja huo

Matokeo hayo yameipandisha Ndanda Fc mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi baada ya kujikusanyia alama 43

Yanga yenye alama 74, imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama nane dhidi ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili ikijikusanyia alama 66

Simba yenye michezo mingi ya viporo, inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 60