Simba kusaka ushindi wa 12 mfululizo Bukoba

Msafara wa wachezaji 18 wa kikosi cha Simba unaondoka leo Ijumaa asubuhi kuelekea Kagera tayari kuwakabili wenyeji wao Kagera Sugar kwenye mchezo utakaopigwa uwanja wa Kaitaba kesho Jumamosi

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wengine wanne watasafiri kesho kuungana na wenzao wanaoondoka leo

Ni beki Paschal Wawa pekee ambaye hakujumishwa kwenye safari hiyo ya kanda ya ziwa kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya nyonga

Baada ya kushinda michezo yote 11 iliyopita na kuweka rekodi mpya kwenye ligi, Simba itakuwa inasaka ushindi wa 12 dhidi ya Kagera Sugar ambayo msimu uliopita ndio timu pekee iliyopata ushindi dhidi ya Simba

Kesho Simba itaingia dimba la Kaitaba ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa bao 1-0 kwenye mchezo ambao ulishuhudiwa na Rais Magufuli msimu uliopita