
Kaya amesema baada taratibu zote za kishasheria kukamilishwa, Beno atakuwa huru kuendelea na maisha yake ya soka mahali pengine
“Suala la Beno lipo katika sheria zaidi, Yanga na Beno walishaachana kwa sababu angekuwa bado anahitajiwa kufanya kazi Yanga sidhani mpaka leo kama angekuwa nje ya timu,” Kaya ameiambia UFM
“Sidhani kama ni sawa kulizungumzia suala ambalo tayari limeshapita”
“Taratibu nyingine za kumalizana zipo nyuma ya pazia tutamalizana na ataendelea na maisha yake kama ambavyo sasa hivi anavyoendelea na maisha yake na Yanga inaendelea na maisha yake”
Beno aliondolewa kikosini mwishoni mwa mwaka jana baada ya kufanya mgomo uliosababisha mgogoro baina yake na kocha Mwinyi Zahera