Aussems ameipaisha Simba, asubiri kusaini mkataba mpya

Wakati alipokabidhiwajukumu la kuinoa Simba mwanzoni mwa msimu, Patrick Aussems alipewa masharti mawili; moja ni kuipeleka Simba hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na pili ni kutetea ubingwa ligi kuu

Aussems amekamilisha sharti la kwanza na kuvuka malengo baada ya kufanikiwa kuivusha Simba hadi robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa

Sharti lililobaki ni la kutetea ubingwa wa ligi kuu, sharti ambalo nalo anaelekea kulikamilisha

Mbelgiji huyo aliyechukua nafasi ya Pierre Lechantre, hakuna shaka atapewa mkataba mpya kuendelea kuinoa Simba kutokana na mafanikio aliyoipatia timu hiyo msimu huu

Mkataba wake na Simba aliosaini msimu uliopatita utamalizika mwishoni mwa msimu