Simba Queens yaiandalia kipigo Yanga Princess leo

Wakinadada wa Simba Queens leo watashuka kwenye uwanja wa Karume kupepetana na watani zao wa jadi Yanga Princess katika mchezo wa ligi kuu ya Wanawake, Serengeti Lite

Simba Queens inayoshika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo, imepania kuendeleza umwamba dhidi ya wapinzani wao hao ambao wanashika nafasi ya saba

Katika mchezo wa raundi ya kwanza Simba Queens iliibamiza Yanga Princess mabao 7-0

JKT Queens inaongoza ligi ikiwa imejikusanyia alama 45 ikiwa imeshinda michezo yake yote.

Mlandizi Queens inashika nafasi ya pili ikiwa imejikusanyia alama 32 sawa na Alliance Girls timu hizo zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa

Simba Queens iko nafasi ya nne ikiwa na alama 31 wakati Yanga Princess inashika nafasi ya saba ikiwa na alama 19