Nyoni augua ghafla, kuikosa Alliance Fc

Simba imepata pigo baada ya beki kiraka Erasto Nyoni kuugua ghafla hivyo atakosa mchezo wa kesho dhidi ya Alliance Fc

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amethibitisha kuwa Nyoni hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani kuikabili Alliance Fc

Nyoni anaungana na beki Paschal Wawa ambaye hakusafiri jijini Mwanza kutokana na majeruhi yanayomkabili