
Mchezo huo utapigwa kesho Jumanne, April 23 katika uwanja huo
Simba ilitua Mwanza mapema jana ikitokea Kagera ambako ilipoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar kwa kuchapwa mabao 2-1
Katika mazoezi hayo yaliyosimamiwa na kocha Patrick Aussems, Simba iliwaruhusu kukaa jukwaani mashabiki waliofika kuwashuhudia mabingwa hao watetezi
Kuelekea mchezo huo, Aussems amesema wanatarajia kupata upinzani mkali kutoka kwa Alliance Fc kutokana na ubora wa kikosi cha timu hiyo
Hata hivyo amesema Simba inahitaji kushinda mchezo huo hasa baada ya kupoteza mchezo uliopita
“Tunajua haitakuwa mechi rahisi sababu Alliance ni timu nzuri lakini sisi tumepoteza mchezo Bukoba na kesho tunataka alama tatu,” amesema Aussems
“Tunajua kwanini tulipoteza na tumejiandaa kwa hilo na ninaamini kesho tutakuwa vizuri.”