Simba Queens yaifumua Yanga Princess 5-1

Wanamama wa Simba Queens leo wameendeleza ubabe kwa watani zao Yanga Princess baada ya kuwafumua mabao 5-1 katika mchezo wa ligi kuu ya Wanawake, Serengeti Lite uliopigwa uwanja wa Karume

Magoli ya Simba Queens yalipachikwa na Opah Clement aliyefunga mabao mawili, Mwanahamisi Omary, Joele Bukulu na Amina Ramadhani na goli pekee la Yanga Princess likifungwa na Fausta Thomas

Huu ni ushindi wa pili kwa Simba Queens dhidi ya watani zao, wakipata ushindi wa mabao 7-0 katika mchezo wa duru ya kwanza wa ligi hiyo ya Wanawake