Zahera aipania Azam Fc

Kikosi cha Yanga leo kimeendelea na mazoezi kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa April 29 2019 katika uwanja wa Taifa

Muda wa mchezo huo utapigwa saa kumi kamili jioni

Wachezaji wote wa Yanga wako katika hali nzuri ambapo Daktari wa timu hiyo Dk Edward Bavu amesema hakuna majeruhi

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema mchezo dhidi ya Azam Fc hautakuwa mwepesi lakini una umuhimu wa kipekee kwa Yanga kupata ushindi ili kuwa na nafasi ya kutwaa ubingwa

“Najua wazi mechi yetu na Azam FC itakuwa ngumu na ya nguvu kwetu kwa sababu sisi wote tunataka tushinde mechi hiyo ili tuzidi kujiwekea mazingira mazuri katika ligi,” amesema

“Tunajiandaa vizuri ili tushinde tuwaache mbali wapinzani wetu, hii ni mechi ambayo tunahitaji matokeo zaidi na tutapambana kwa ajili ya hilo”