FT : Alliance 0-2 Simba

Simba imeendeleza mawindo yake ya ubingwa wa pili mfululizo ambapo leo imefanikiwa kuibomoa Alliance Fc mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa CCM Kirumba

Simba iliyokuwa na mabadiliko katika kikosi kilichoanza, ilijipatia bao la kuongoza kwenye dakika ya 21 kupitia kwa kiungo fundi Haruna Niyonzima

Bao la pili liliwekwa kambani na Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 75

Okwi alianzia benchi kwenye mchezo huo ambapo aliingia katika dakika ya 64 kuchukua nafasi ya Adam Salamba

Hilo lilikuwa bao la tisa kwa Okwi msimu huu sasa akiwa amefunga katika michezo yote miwili iliyopita

Matokeo hayo yameifanya Simba ifikishe alama 63 sasa ikiwa nyuma ya Azam Fc kwa tofauti ya alama tatu

Ushindi katika mchezo unaofuata dhidi ya KMC utaipaisha Simba hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi

Simba itaendelea kubaki jijini Mwanza kusubiri mchezo dhidi ya KMC ambao utapigwa keshokutwa Alhamisi, katika uwanja wa CCM Kirumba