
Simba iliyokuwa na mabadiliko katika kikosi kilichoanza, ilijipatia bao la kuongoza kwenye dakika ya 21 kupitia kwa kiungo fundi Haruna Niyonzima
Bao la pili liliwekwa kambani na Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 75
Okwi alianzia benchi kwenye mchezo huo ambapo aliingia katika dakika ya 64 kuchukua nafasi ya Adam Salamba
Hilo lilikuwa bao la tisa kwa Okwi msimu huu sasa akiwa amefunga katika michezo yote miwili iliyopita
Matokeo hayo yameifanya Simba ifikishe alama 63 sasa ikiwa nyuma ya Azam Fc kwa tofauti ya alama tatu
Ushindi katika mchezo unaofuata dhidi ya KMC utaipaisha Simba hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi
Simba itaendelea kubaki jijini Mwanza kusubiri mchezo dhidi ya KMC ambao utapigwa keshokutwa Alhamisi, katika uwanja wa CCM Kirumba