Djuma yamkuta Rwanda, atimuliwa As Kigali

Aliyewahi kuwa kocha Msaidizi wa Simba Masudi Djuma ambaye alikuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo, ametimuliwa klabu ya AS Kigali aliyokuwa akiifundisha

Djuma alijiunga na AS Kigali mwezi Oktoba mwaka jana baada ya uongozi wa Simba kuvunja mkataba wake akituhumiwa kumfanyia hujuma kocha Patrick Aussems

Djuma ameinoa AS KIgali kwa muda wa miezi saba tu akitimuliwa baada ya kuiongoza timu hiyo katika michezo mitano iliyopita bila ya kupata ushindi