Simba yakamilisha maandalizi ya kuikabili KMC

Kikosi cha Simba leo asubuhi kimefanya mazoezi ya mwisho kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya KMC

Mchezo huo utapigwa kesho Alhamisi kwenye uwanja wa CCM Kirumba

Simba ilishuka katika uwanja huo huo jana kuikabili Alliance Fc katika mchezo ambao Simba ilishinda kwa mabao 2-0

Baada ya mazoezi hayo yaliyosimamiwa na kocha Patrick Aussems, wachezaji walipewa mapumziko kusubiri mchezo huo wa kesho

Ratiba ya mabingwa hao watetezi haitoi nafasi kwa wachezaji kupata mapumziko ya kutosha hivyo benchi la ufundi kulazimika kupunguza muda wa mazoezi ili kuwapumzisha wachezaji