Azam Fc vs Yanga kupigwa uwanja wa Uhuru

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Azam Fc dhidi ya Yanga ambao awali ulipangwa kupigwa uwanja wa Taifa, sasa umehamishiwa uwanja wa Uhuru

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wamepokea barua kutoka TFF inayowaelekeza sababu ya mchezo huo kuhamishiwa uwanja wa Uhuru ni kutoa nafasi kwa uwanja wa Taifa kufanyiwa ukarabati baada ya kumalizika mchezo wa fainali AFCON U17 utakaopigwa April 28 2019

Kikosi cha Yanga kinaendelea kujifua kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa Jumatatu, April 29 2019 saa kumi kamili jioni

Uwanja wa Uhuru ulifanyiwa ukarabati kabla ya kuanza kwa michuano ya vijana ya AFCON ambapo nyasi bandia za uwanja huo zilibadilishwa