Mshambuliaji Emmanuel Okwi ameendeleza rekodi ya kuzifumania nyavu katika ligi hiyo leo akiitanguliza Simba kwa bao safi alilofunga kwenye dakika ya 23
Okwi amefunga kwenye mchezo wa tatu mfululizo sasa akifikisha mabao 10
KMC iliyokuwa bora katika kipindi cha pili ilisawazisha bao hilo kupitia kwa Hassani Kabunda kwenye dakika ya 57 kabla nahodha John Bocco hajaihakikishia Simba alama tatu muhimu kwa kuifungia bao la ushindi kupitia mkwaju wa penati katika dakika ya 82
Hiyo ilikuwa penati ya pili kwa Simba kwenye mchezo huo. Meddie Kagere alikosa penati ya kwanza kwenye dakika ya 60
Ushindi huo umeipandisha Simba mpaka nafasi ya pili baada ya kufikisha alama 66 na kuwa sawa na Azam Fc
Hata hivyo Simba ina mtaji mkubwa wa mabao
Sasa zimebaki alama nane tu kuifikia Yanga kileleni, Simba ikihitaji kushinda michezo mitatu tu ili kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi
Kikosi cha Simba kinaelekea mkoani Mara kuikabili Biashara United, mchezo utapigwa keshokutwa Jumamosi, April 27 2019