Simba yajifua Mara

Kikosi cha Simba leo jioni kimefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume wilayani Musoma kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja huo

Msafara wa Simba uliwasili mkoani Mara mapema leo na kupokewa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa na shauku ya kuwaona mabingwa hao wa nchi