Wachezaji wafika mazoezini kuendelea na maandalizi ya kuikabili Azam Fc

Wachezaji wote leo wamefika mazoezini kuendelea na maandalizi ya mchezo dhidi ya Azam Fc utakaopigwa Jumatatu, April 29 kwenye uwanja wa Uhuru

Jana wachezaji hao waligoma kufanya mazoezi wakishinikiza waonane na uongozi wa Yanga ili kujua hatma ya madai yao ya mishahara na fedha za usajili

Wagoma tena

Licha ya kufika mapema mazoezini, wachezaji wa kikosi cha kwanza, waligoma kufanya mazoezi wakiwasubiri viongozi wafanye nao kikao

Kocha Zahera alilazimika kutumia Yanga B kuendelea na program ya mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Azam