
Simba imefikisha alama 69 sasa ikitofautiana na Yanga kwa tofauti ya alama tano tu huku kibindoni ikiwa na michezo mitano ya viporo
Shukrani za kipekee zimwendee nahodha John Bocco aliyefunga mabao yote mawili kwenye kipindi cha kwanza na kuihakikishia Simba alama tatu muhimu
Bocco amefikisha mabao 14 akichupa mpaka nafasi ya tatu kwenye orodha ya vinara wa mabao nyuma ya Makambo mwenye mabao 15
Aidha Bocco amefikisha idadi ya mabao aliyofunga msimu uiliopita
Katika mchezo huo Simba ilipata pigo baada ya kiungo wake Haruna Niyonzima kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi
Simba imemaliza michezo ya kanda ya ziwa na sasa inarejea jijini Dar es salaam ambapo Jumanne itachuana na JKT Tanzania, mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru