Mashabiki wa Simba Mara ‘mmetisha’

Mapokezi na sapoti iliyopata Simba mkoani Mara ni ya kipekee na hakika watu wa Musoma wanastahili pongezi kwa ‘vibe’ la maana waliloonyesha leo

Simba haikuwa imefika Mara katika kipindi cha miaka 15 kutokana na mkoa huo kukosa timu ya ligi kuu, makaribisho iliyopata yanadhihirisha ukubwa wa Simba nchini Tanzania kwa sasa

Baada ya mchezo wa leo kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka kesho kurejea jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya JKT Tanzania