Mashabiki mapemaa uwanja wa Karume

Leo saa kumi kamili jioni mabingwa wa nchi Simba watashuka kwenye uwanja wa Karume kuchuana na Biashara United katika mchezo wa kiporo wa ligi kuu ya Tanzania

Simba ilipowasili mkoani Mara jana, shamrashamra za mashabiki zilikuwa kubwa hali hiyo imeendelea mpaka leo ambapo mashabiki walianza kuingia uwanjani tangu saa tatu asubuhi

Mpaka kufika saa 10 jioni huenda mashabiki ambao watachelewa wakalazimika kurudi nyumbani kuushuhudia mchezo huo runingani kwani mpaka sasa uwanja wa Karume unaelekea kujaa

Mashabiki wana shauku ya kuishuhudia Simba ambayo imetua mkoani Mara kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 15