Simba yasaka alama tatu dhidi ya Biashara United leo

Kikosi cha mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba kiko mkoani Mara ambapo leo kitashuka kwenye uwanja wa Karume kupepetana na wenyeji wao Biashara United

Baada ya ushindi dhidi ya Alliance na KMC, Simba imeingia Mara ikiwa na shauku yas kupata alama nyingine tatu ili kujisogeza zaidi kileleni mwa msimamo wa ligi

Biashara United imeweka hadharani viingilio vya mchezo huo ambapo VIP ni Tsh 20,000/- Mzunguuko Tsh 5,000/- huku watoto wakiwekewa kiingilio cha Tsh 3,000/-

Mchezo utapigwa kuanzia saa kumi kamili jioni

Kila la kheri mabingwa wa nchi…!