Niyonzima aomba radhi

Kiungo fundi Haruna Niyonzima amewaomba radhi kwa uongozi wa klabu ya Simba pamoja na mashabiki wa timu hiyo kufuatia kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo wa jana dhidi ya Biashara United, mchezo ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Niyonzima amesema anajutia tukio alilofanya ambalo lilisababisha apewe kadi nyekundu

“Ulikua mchezo wenye presha kubwa sana ukizingatia tulihitaji sana matokeo kuliko chochote,” amesema

“Iliniumiza sana kutoka uwanjani nikiacha timu yangu pungufu. Niombe radhi kwa klabu yangu mashabiki zetu waliosafiri mpaka Mara na pia wale wote mliokua majumbani mkitizama kupitia televisheni”

“Nilichofanya hakikuwa bora kwa ustawi wa mpira wetu samahani wote mliokwazika, tutapambana mpaka tone la mwisho kwajili ya ubingwa”