Simba yaondoka Mwanza kurejea Dar

Kikosi cha Simba kimeondoka leo jijini Mwanza kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na ratiba ya michezo ya ligi kuu ambapo keshokutwa Jumanne itachuana na JKT Tanzania katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru

Simba imemaliza salama ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa ikifanikiwa kushinda michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya kuzifuata Mbeya City na Tanzania Prisons