Kapombe anakaribia kurejea kisosini Simba

Uongozi wa Simba umethibitisha kuwa beki wake kiraka Shomari Kapombe anakaribia kurejea kikosini baada ya kuanza mazoezi mepesi

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema Kapombe amepona majeraha ya goti na tayari ameanza mazoezi ya gym ikiwa ni hatua ya mwanzo kabla ya kurejea dimbani

“Tunashukuru beki wetu Shomari Kapombe amepona majeraha ya goti yaliyomuweka nje kwa muda mrefu. Hivi sasa anafanya mazoezi ya Gym ili kuurejesha mwili katika hali yake kabla ya kuanza mazoezi ya mpira,” amesema

Kapombe amekuwa nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha ya goti aliyopata nchini Afrika Kusini wakati akiitumikia timu ya Taifa

Licha ya beki huyo kuanza kujifua, kuna uwezekano mdogo kwake kucheza mechi zilizobaki