Wagombea Yanga kuanza kampeni Jumanne

Wagombea waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika klabu ya Yanga, wanatarajiwa kuanza rasmi kampeni kesho Jumanne, April 30 2019

Kampeni zitaanza baada ya muda wa rufaa kwa wagombea walioenguliwa kupita huku mgombea mmoja kati ya 15 ambao majina yao yalienguliwa, amekata rufaa

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahella amesema rufaa ya mgombea huyo wa nafasi ya Ujumbe, Rodgers Gumbo itasikilizwa kesho

Uchaguzi Mkuu wa Yanga kuwapata viongozi wapya watakoiongoza timu hiyo kwa kipindi cha miaka minne utafanyika Jumapili, May 05 2019

Hii hapa orodha ya wagombea wote waliopitishwa;

Mwenyekiti

1. Baraka Igagungula (ME)
2. Dr. Jonas Tiboroha (ME)
3. Elias Mwanjala (ME)
4. Dr. Mbette Mshindo Msola (ME)

Makamu Manyekiti

1. Fredrick Mwakalebela (ME)
2.Jannet Mbene (KE)
3. Titus Osoro (ME)
4. Yono Kevela (ME)

Wajumbe

1. Saady Mohamed Khimji (ME)
2. Hassan H. Yahaya (ME)
3. Arafat Hajji (ME)
4. Suma Mwaitenda (KE)
5. Hamad Islam (ME)
6. Dominick Albinus (ME)
7. Sharifu Amour Makosa (ME)
8. Eng. Bahati F. Mwaseba (ME)
9. Eng. Leonard Marango (ME)
10. Haruna H. Batenga (ME)
11. Athanas Kazinghe (ME)
12. Ramadhan Said (ME)
13. Salim Rupia (ME)
14. Dominick Francis (ME)
15. Sharifu Amir (ME)
16. Benjamin Mwakasendo (ME)
17. Christopha Kashiririka (ME)
18. Ally Msigwa (ME)
19. Frank K. Kamugisha (ME)
20. Said Kambi (ME)
21. Silvester Haule (ME)

NB : Rufaa ya mgombea mmoja wa nafasi ya Ujumbe Rodgers Gumbo itasikilizwa kesho Jumanne April 30 2019