Nimepata maumivu ya kawaida – Gadiel

Beki wa kushoto wa Yanga Gadiel Michael Mbaga amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kuwa hali yake inaendelea vizuri

Gadiel alishindwa kuendelea na mchezo leo dhidi ya Azam Fc baada ya kuumia kwenye kipindi cha kwanza na nafasi yake kuchukuliwa na Jaffar Mohammed

Gadiel amesema alipata mshtuko uliosababisha maumivu ya misuli. Amesema akipata mapumziko ya siku tatu hadi nne atakuwa sawa

“Nimepata maumivu ya kawaida ya misuli, mapumziko ya siku tatu hadi nne yatanisaidia kurejea katika hali yangu ya kawaida,” amesema

Yanga inakabiliwa na mchezo mwingine wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa Alhamisi, May 02 kwenye uwanja wa Taifa