Ninja, Chikupe wawatuliza Chirwa na Ngoma

Washambuliaji wa zamani wa Yanga Obrey Chirwa na Donald Ngoma ambao wanakipiga katika klabu ya Azam Fc leo wameshindwa kufurukuta mbele ya waajiri wao wa zamani wakikubali kipigo cha bao 1-0

Walinzi wawili wa kati wa Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Andrew Vicent ‘Dante’ leo walikuwa na kazi maalum ya kuhakikisha washambuliaji hao hawasababishi madhara

Hakika kazi hiyo wameifanya kwa ustadi mkubwa kwani walifanikiwa ‘kuwaweka mifukoni’ washambuliaji hao

Wakati Ngoma alipata mwanya wa kufunga bao lililokataliwa na mwamuzi baada ya kumfanyia madhambi Chikupe, nafasi pekee aliyopata Chirwa kwenye kipindi cha kwanza iliokolewa kwa ustadi mkubwa na kipa Klaus Kindoki

Ushindi wa Yanga leo umechangiwa kwa kiasi kikubwa na umakini wa walinzi hao na wachezaji wote kwa ujumla ambao walikuwa na nidhamu ya hali ya juu katika ulinzi

Licha ya kumiliki mpira kwa muda mwingi, Azam Fc ilikosa mbinu ya kuipenya ngome ya Yanga