
Simba ililazimika kusubiri hadi dakika za nyongeza kujipatia bao la ushindi lililowekwa kambani na Hassani Dilunga huku pasi ya bao ikitotewa na Emmanuel Okwi
JKT Tanzania walitoa upinzani mkali kwa mabingwa hao watetezi lakini uzoefu na kujitolea kwa wachezaji kulifanikisha Simba kuchukua alama zote tatu dakika za majeruhi
Ushindi huo unaifanya Simba izidi kuikaribia Yanga baada ya kufikisha alama 72 ikitofautiana kwa alama tano tu na Yanga inayoongoza ligi




Kituo kinachofuata ni Mbeya ambapo May 03 Simba itashuka dimba la Sokoine kuikabili Mbeya City
