Kapombe aitwa Stars, yaelezwa atakuwa ‘fiti’ kucheza AFCON 2019

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Emmanuel Amunike ameonyesha imani kwa beki wa Simba Shomari Kapombe baada ya kumjumuisha kwenye kikosi chake cha awali ambacho baadae kitatenganishwa kwa ajili michuano ya AFCON 2019 na michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wa ndani

Kapombe aliumia Afrika Kusini mwezi Novemba mwaka jana wakati akiitumikia timu Taifa.

Amekuwa nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha ya goti ambayo yalihitaji kufanyiwa upasuaji

Baada ya kupona majeraha, Kapombe tayari ameanza mazoezi mepesi na inaelezwa ataweza kushiriki michuano ya AFCON itakayofanyika mwezi ujao nchini Misri

Hii ni habari njema kwa Simba ambayo huenda ikamtumia beki huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja katika baadhi ya michezo yake ya kumaliza msimu