
Kapombe aliumia Afrika Kusini mwezi Novemba mwaka jana wakati akiitumikia timu Taifa.
Amekuwa nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha ya goti ambayo yalihitaji kufanyiwa upasuaji
Baada ya kupona majeraha, Kapombe tayari ameanza mazoezi mepesi na inaelezwa ataweza kushiriki michuano ya AFCON itakayofanyika mwezi ujao nchini Misri
Hii ni habari njema kwa Simba ambayo huenda ikamtumia beki huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja katika baadhi ya michezo yake ya kumaliza msimu