Sita Simba waitwa Stars kwa ajili ya AFCON na CHAN

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Emmanuel Amunike leo ametangaza majina ya wachezaji 40 wanaounda kikosi cha timu ya Taifa ambacho kitashirikia michuano ya AFCON 2019 itakayofanyika mwezi ujao nchini Misri pamoja na michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wa ndani

Katika kikosi hicho, wachezaji wa Simba Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein, Erasto Nyoni, Jonas Mkude na John Bocco wamejumuishwa