
Baada ya juzi kuichapa Azam Fc bao 1-0, Yanga itakuwa na nafasi ya kuzidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi kama itaibuka na ushindi kwenye mchezo huo
Mabingwa hao wa kihistoria wamesalia na michezo mitano kabla ya kumalizika kwa ligi, kama watashinda yote watafikisha alama 92
Bado Yanga haiwezi kuondolewa katika mbio za ubingwa kwani wapinzani wao Simba bado watahitaji kupata matokeo katika michezo yao10 iliyobaki ili waweze kutete ubingwa
Baada ya mchezo wa kesho Yanga itaelekea mkoani Iringa tayari kwa mchezo wa nusu fainali kombe la FA dhidi ya Lipuli Fc utakaopigwa May 06 2019