Ajib ajumuishwa kikosi cha Stars

Hatimaye kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Emmanuel Amunike amemjumuisha nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib kwenye kikosi cha timu ya Taifa kitakachoshiriki michuano ya AFCON itakayofanyika mwezi ujao nchini Misri pamoja na michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wa ndani

Kikosi hicho chenye wachezaji 39 pia kimewajumuisha Gadiel Michael, Kelvin Yondani na Feisal Salum kutoka klabu ya Yanga