Makambo awafikia Aiyee, Kagere

Bao alilofunga Heritier Makambo katika mchezo dhidi ya Tanzania Prisons limemfanya mshambuliaji huyo afikishe mabao 16 na kuwafikia Salum Aiyee wa Mwadui Fc na Meddie Kagere wa Simba

Leo Makambo ameiongoza Yanga kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons

Mshambuliaji huyo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, anayo nafasi ya kuibuka mfungaji bora msimu huu kama ataweza kuitumia vyema michezo minne iliyobaki kujiongezea mabao

Michezo iliyobaki ni dhidi ya Ruvu Shooting, Mbeya City, Biashara United na Azam Fc

Ni mchezo mmoja tu dhidi ya Biashara United ambao utapigwa nje ya jiji la Dar es salaam