Simba yawasili salama Mbeya

Msafara wa kikosi cha Simba umewasili salama mkoani Mbeya tayari kwa michezo miwili ya ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Simba iliondoka jijini Dar es salaam mchana wa leo Alhamisi kwa usafiri wa Ndege

Kesho May 03 itacheza mchezo wa kwanza dhidi ya Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine na siku mbili baadae kurudi tena katika uwanja huo kuikabili Tanzania Prisons

Prisons iko jijini Dar es salaam ambapo leo imecheza na Yanga na kufungwa mabao 2-1, itachuana na Simba May 05