Rekodi ya mabao Simba inatisha

Simba imeendelea ‘kuzikimbiza’ timu nyingine zinazoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara, ikiongoza kwa kufunga mabao

Mabao mawili yaliyoiwezesha Simba kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Mbeya City leo, yameifanya timu hiyo iwe imefunga mabao 60

Meddie Kagere sasa ndiye kinara wa kuzifumania nyavu akiwa ametupia kambani mabao 17 akiwaacha washindani wake Salum Aiyee (16) na Heritier Makambo (16)

Katika mabao 60 yaliyofungwa mpaka sasa, Kagere, Okwi na Bocco wamechangia mabao 41

Kagere (17), Okwi (10) na Bocco (14)

Lakini pia Simba ndio timu iliyoruhusu mabao machache zaidi mpaka sasa ikiwa imefungwa mabao 12 tu. Azam Fc inafuatia ikiwa imeruhusu mabao 19

Simba inakaribia kutetea ubingwa wake ikihitaji kushinda michezo sita kati ya tisa iliyobaki

Baada ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa, Simba itarejea jijini Dar es salaam ambako itacheza michezo sita katika dimba la Taifa/Uhuru

Huenda ikatangaza ubingwa kupitia michezo hiyo