Mastaa kibao waalikwa ‘Gala Dinner’ May 11

Siku ya Jumamosi ya May 11 2019 Yanga imepanga kuandika historia jijini Dar es salaam katika hafla maalum ya chakula cha jioni iliyoandaliwa Kamati ya Uhamishaji wa michango inayoongozwa na Mh Anthony Mavunde

Hafla hiyo ambayo itatumika ‘kuijaza Yanga mapesa’, itawashirikisha wadau wake mbalimbali ambao kwa umoja wao wamedhamiria kuirejesha heshima ya timu hiyo

Mwanamuziki Ali Kiba ni miongoni mwa watu maarufu watakaohudhuria hafla hiyo itakayofanyika Hoteli ya Serena kuanzia saa 12 jioni

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh Jokate Mwegelo, Wema Sepetu, Jackline Wolper, Batuli, Vicent Kigosi na Steve Nyerere nao watakuwepo