Hafla hiyo ambayo itatumika ‘kuijaza Yanga mapesa’, itawashirikisha wadau wake mbalimbali ambao kwa umoja wao wamedhamiria kuirejesha heshima ya timu hiyo
Mwanamuziki Ali Kiba ni miongoni mwa watu maarufu watakaohudhuria hafla hiyo itakayofanyika Hoteli ya Serena kuanzia saa 12 jioni
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh Jokate Mwegelo, Wema Sepetu, Jackline Wolper, Batuli, Vicent Kigosi na Steve Nyerere nao watakuwepo





