Simba inayoshika nafasi ya pili baada ya kujikusanyia alama 72, inahitaji ushindi katika michezo saba tu ili kuubakisha ubingwa Msimbazi
Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji wa timu hiyo wako katika hali nzuri tayari kwa mchezo huo
“Timu imewasili salama mkoani Mbeya tayari kwa mchezo. Tunafahamu hautakuwa mchezo mwepesi lakini wachezaji wetu watapambana kuhakikisha tunaondoka na alama zote tatu,” amesema
Katika mchezo wa leo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye aliumia kwenye mchezo uliopita dhidi ya JKT Tanzania
Wengine watakaokosekana ni Asante Kwasi, Paschal Wawa na Shomari Kapombe
Baada ya mchezo huo Simba itaendelea kubaki mkoani Mbeya ambapo keshokutwa May 05 itachuana na Tanzania Prisons