Simba yasaka alama tatu dhidi ya Mbeya City leo

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wako mkoani Mbeya ambapo leo watashuka dimba la Sokoine kuwakabili wenyeji wao Mbeya City

Simba inayoshika nafasi ya pili baada ya kujikusanyia alama 72, inahitaji ushindi katika michezo saba tu ili kuubakisha ubingwa Msimbazi

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji wa timu hiyo wako katika hali nzuri tayari kwa mchezo huo

“Timu imewasili salama mkoani Mbeya tayari kwa mchezo. Tunafahamu hautakuwa mchezo mwepesi lakini wachezaji wetu watapambana kuhakikisha tunaondoka na alama zote tatu,” amesema

Katika mchezo wa leo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye aliumia kwenye mchezo uliopita dhidi ya JKT Tanzania

Wengine watakaokosekana ni Asante Kwasi, Paschal Wawa na Shomari Kapombe

Baada ya mchezo huo Simba itaendelea kubaki mkoani Mbeya ambapo keshokutwa May 05 itachuana na Tanzania Prisons