Yanga yatua Iringa kibabe, yaipania Lipuli Fc

Vinara wa ligi kuu Tanzania Bara Yanga waliwasili mkoani Iringa jana jioni tayari kwa mchezo wa nusu fainali kombe la FA dhidi ya Lipuli fc

Mchezo huo utapigwa Jumatatu, May 06 uwanja wa Samora

Yanga inayosaka nafasi ya kurejea kwenye michuano ya Kimataifa msimu ujao, imepania kushinda mchezo huo ili kutinga fainali ambapo kama ikifanikiwa, itachuana na Azam Fc

Msafara wa Yanga umejumuisha wachezaji 24 ambao leo wataanza maandalizi ya mchezo huo mkoani Iringa