
Bao pekee la Simba lilipatikana kwenye kipindi cha kwanza likiwekwa kambani na Emmanuel Okwi katika dakika ya 11 baada ya shambulizi la kushitukiza
Ushindi huo umeendelea kuisogeza Simba kileleni baada ya kufikisha alama 78 sasa ikihitaji alama mbili tu kuweza kuifikia Yanga
Yanga ina alama 80 ikiwa imecheza michezo minne zaidi ya Simba pia
Okwi ameendelea kuwasogelea vinara wa mabao leo akifikisha mabao 11
Mchezo unaofuata ni dhidi ya Coastal Union na utapigwa May 08 kwenye uwanja wa Taifa