FT : Prisons 0-1 Simba

Simba imeendelea kuukaribia ubingwa wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Tanzania Prisons bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya

Bao pekee la Simba lilipatikana kwenye kipindi cha kwanza likiwekwa kambani na Emmanuel Okwi katika dakika ya 11 baada ya shambulizi la kushitukiza

Ushindi huo umeendelea kuisogeza Simba kileleni baada ya kufikisha alama 78 sasa ikihitaji alama mbili tu kuweza kuifikia Yanga

Yanga ina alama 80 ikiwa imecheza michezo minne zaidi ya Simba pia

Okwi ameendelea kuwasogelea vinara wa mabao leo akifikisha mabao 11

Mchezo unaofuata ni dhidi ya Coastal Union na utapigwa May 08 kwenye uwanja wa Taifa