
Simba imejiweka katika mazingira mzuri ya kutetea ubingwa wake baada ya kuondoka na alama zote sita mkoani Mbeya
Mbeya City na Tanzania Prisons zilikuwa zikiangaliwa kuwa na uwezo wa ‘kuitibulia’ Simba hesabu zake kuelekea ubingwa
Simba imesalia na michezo nane, michezo sita itapigwa jijini Dar es salaam kunako uwanja wa Taifa au Uhuru
Simba itatoka nje ya jiji kuzifuata Singida United na Mtibwa Sugar (mchezo wa pili) wakati Coastal Union, Kagera Sugar, Azam Fc, Mtibwa Sugar(mchezo wa kwanza), Ndanda na Biashara United zote zitaifuata Simba ‘majinjioni’ uwanja wa Taifa
Simba huenda ikarejea rasmi kileleni mwa msimamo wa ligi Jumatano May 08 itakapocheza na Coastal Union mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa/Uhuru