Viongozi Yanga watua Iringa kuongeza nguvu

Viongozi wapya wa klabu ya Yanga wametimiza ahadi baada ya kuwasili mkoani Iringa kuiunga mkono timu yao inayoshuka uwanja wa Samora kuikabili Lipuli Fc katika mchezo wa nusu fainali kombe la FA

Msafara wa viongozi hao umeongozwa na Mwenyekiti Dk Mbette Mshindo Msolla na Makamu Mwenyekiti Fredrick Mwakalebela pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji

Yanga imeweka mkazo katika kuhakikisha wanatinga fainali na baadae kutwaa taji la kombe la FA ili kupata nafasi ya kushiriki michuano ya CAF msimu ujao