
Lakini mpaka sasa wao watatu, nahodha John Bocco, Meddie Kagere na Emmanuel Okwi wamefunga mabao 48 kati ya 69 yaliyofungwa na Simba msimu huu
Kagere ndiye anayeshikilia usukani wa mbio za kuwania kiatu cha dhahabu akiwa amefunga mabao 20 wakati Bocco na Okwi wote wamefunga mabao 14
Msimu huu Simba tayari imeshaweka rekodi tatu muhimu; moja ni timu iliyofunga mabao mengi zaidi kwenye mchezo mmoja (8-1) na pili ni timu iliyofunga mabao mengi zaidi kwa ujumla mpaka sasa (69) na tatu ni timu iliyoruhusu mabao machache (13)
Kama itashinda michezo yote saba ilyobaki, Simba itaweka rekodi ya kufikisha alama 102. Mpaka sasa inahitaji kushinda michezo minne tu ili kuweza kutetea ubingwa