Simba kuendelea na msako wa ubingwa uwanja wa Uhuru leo

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba leo wanashuka uwanja wa Uhuru kuikabili Kagera Sugar ukiwa ni mchezo wa ligi raundi ya 35

Mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka, utakuwa wa kisasi kwa Patrick Aussems na vijana wake baada ya kupoteza mchezo wa duru ya kwanza

Leo Simba imepania kumaliza ‘uteja’ kwa Kagera Sugar inayonolewa na kocha Meckie Mexime

Mexime ameshinda michezo miwili iliyopita dhidi ya Simba

Msimu uliopita Kagera Sugar iliharibu sherehe ya Simba kukabidhiwa ubingwa baada ya kushinda kwa bao 1-0 mbele ya Rais Magufuli na viongozi waandamizi wa Serikali na klabu ya Simba

Lakini pia msimu huu Kagera Sugar ilishinda mchezo uliopigwa uwanja wa Kaitaba

Kikosi cha timu hiyo kiko jijini Dar es salaam tangu Jumatatu kikijiwinda na mtanange huo wa kukata na shoka

Matokeo ya ushindi kwa Simba yatazidi kuwasogeza karibu ya ubingwa wa pili mfululizo kwani wanahitaji kushinda michezo minne tu kati ya saba iliyobaki