Simba yaita mashabiki uwanja wa Uhuru

Uongozi wa klabu ya Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Uhuru leo wakati mabingwa hao wa nchi watakapokuwa wakichuana na Kagera Sugar

Simba inahitaji ushindi kwenye mchezo huo ili kuendelea kuukaribia ubingwa ambapo wanahitaji kushinda michezo minne tu

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema baada ya kupoteza mchezo wa mkoani Kagera, leo ni zamu ya Wana Msimbazi kufurahi kwenye dimba lao la nyumbani

“Kutesa kwa zamu, zamu yao iliishia Kagera na sisi leo zamu yetu. Wanasimba tujitokeze kwa wingi kuwashangilia wachezaji wetu mwanzo wa mchezo hadi mwisho,” amesema

Licha ya hali ya hewa ya mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es salaam, mchezo huo utapigwa kama ulivyopanga